Fighting Malaria
Published in April 2007
in Zanzibar



Listen to the Interview
in English or Swahili
Windows Media 2.1 MB

Mimi ninaitwa Safia Mohamed, nina miaka thelathini na sita, nimeolewa na nina mtoto mmoja.

Je, wafanya kazi gani ?

Mimi ni mke wa nyumbani. Global Fund nimeisikia. Walipita masheha wakawa wanaandika watoto wote ambao hawajafika miaka mitano. Halafu ikatoka tangazo kwenye redio kwamba neti zitatoka, na sehemu. Ilipofika siku tulichukuwa neti. Sio mbali sana kwa sababu ilitafutwa senta hapa kwetu. Sijui utaratibu uliotumika.

Na umefurahishwa na matokeo ?

Naam, kwa sababu mtoto amepata chandarua cha bure, ni kama zawadi yake. Saa hizi ana miaka sita.

Sasa, ungeweza kuniambia, maisha ya familia yako ama ya jamii imebadilikaje ?

Labda nizungumzie kwa familia ya kwangu. Kwa sababu familia nyengine sitoweza kuijua. Yangu imekuwa ni afadhali, kwa sababu naangalia ule mda mtoto ameenda hospitali. Nikichukulia ameenda hospitali mwezi wa nne wa mwaka jana, na amerudi tena hospitali Februari ya mwaka huu 2007. Na pia siyo kama amerudi hospitali kwamba ana malaria; alipoangaliwa , ni ‘negative’ malaria, isipokuwa tu anasumbuliwa na pumzi. Ni mafanikio.

Kabla ya kupata chandaruwa, alikuwa akienda hospitali mara ngapi?

Alikuwa akienda mara mbili au tatu kwa mwaka. Dawa za malaria, tulikuwa ukienda kituoni hamna. Tunaenda kununua zetu binafsi, lakini kwa wakati huu tunaona kama dawa zinapatikana.

Sasa hivi, hiyo pesa unaitumiaje - na unayo mengine ya kusema?

Siku hizi naitumia pesa kununua malishi bora ya mtoto. Sina chochote- isipokuwa jamii tu- ielewe kwamba ni nini malaria, vipi unapata malaria- kisha watajua namna gani ya kujikinga na malaria.

Country SiteKey Indicators
GLOBAL FUND PROGRAMS IN
ZANZIBAR
View the complete Portfolio of Grants
View Grants by Round:All 1 2 3 4 6 8
HIV/AIDS 
Round 2:Zanzibar AIDS Commission
Round 6:The Ministry of Health and Social Welfare of the Revolutionary Government of Zanzibar
Zanzibar AIDS Commission

Malaria 
Round 1:The Ministry of Health and Social Welfare of the Revolutionary Government of Zanzibar
Round 4:The Ministry of Health and Social Welfare of the Revolutionary Government of Zanzibar
Round 8:Not Defined

TB 
Round 3:The Ministry of Health and Social Welfare, Zanzibar

Total Funding Request:$38,371,247
Approved Maximum*:$24,727,248
* total Approved Funding for Phase 1 & Phase 2